Tuesday, 1 October 2013
Tanzania katika hatua za muhimu za kuanza utekekelzaji wa mradi wa "Single Window System"
Posted on 14:14 by Unknown
Mkurugenzi wa TEKNOHAMA (ICT) wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Ndg. Phares Magesa (kulia) akiongoza ujumbe wa TPA kwenye teleconference na Trade Mark East Africa(TMEA) katikati ni Ndg. Mark wa TMEA na Ndg. Alfred wa TPA .... Tanzania iko katika hatua muhimu ya utekelezaji wa mradi wa "electronic Single Window System" mradi huu utasaidia kuharakisha na kurahisisha mfumo wa mzima wa ufanyaji biashara ya uagizaji(import) na usafirishaji(export) wa bidhaa nje ya nchi.
washindi wa chemsha bongo wapatikana
Posted on 13:30 by Unknown
Washindi wanne kati ya watano waliohitajika wa Chemsha Bongo ya kueleza tairi hili lilivyowekwa hapo wamepatikana baada ya wote kutaja kwa usahihi kwamba upande mmoja (usioonekana) wa hilo tairi ulikatwa kabla ya kuvishwa shinani.
Wadau wengi walijaribu (nasi tumewashukuru kwa kujaribu) na tunawapongeza sana, japo walikosea kusema kuwa tairi liliwekwa hapo tokea mti ukiwa mdogo. Ahsanteni wote kwa kushiriki.
Washindi wetu ni: Frank Msillu,
Waheed Humoud, na amina Anita Daudi.
Tunaomba wadau mlioshinda mtupe anuani zenu kwa njia ile ile mliyojibia swali ili tufanye mipango kuwapatia zawadi za T-shirt za Michuzi Blog 2014 mara tu zitapokuwa tayari.
Huu ni mwanzo tu wa michezo ya Globu ya Jamii ambayo imepania kutoa zawadi za hizo T-shirt kwa wadau mara kwa mara. Hivyo kaeni chonjo...
mtuhumiwa wa mauaji auawa na wananchi makete
Posted on 13:09 by Unknown
Na Edwin Moshi, Makete
Katika hali isiyo ya kawaida wananchi wanaodhaniwa kuwa ni wa kijiji cha Usagatikwa kata ya Tandala wilaya ya Makete mkoani Njombe wameamua kuchukua sheria mkononi kwa kumpiga hadi kumuua Bw. Festo Sigala(44) kwa tuhuma za mauaji
Tukio hilo limetokea Septemba 29 mwaka huu katika kijiji cha Tandala wilayani hapo, baada ya wananchi hao kumfuata mtuhumiwa huyo kwa lengo la kumdhuru kutokana na tuhuma za mauaji ya mwananmke aliyetambulika kwa jina la Furaha Datovu Sanga(37)
Akithibitisha hilo ofisini kwake Mkuu wa polisi(OCD) wilaya ya Makete Alfred Kasonde (Pichani) amesema Bw. Nesco Thobias Chaula mkazi wa kijiji cha Usagatikwa aligundua kupatikana kwa mwili wa marehemu Furaha ambaye aliripotiwa kupotea tangu Mei 15 mwaka huu ambapo alitafutwa bila mafanikio ambapo mwili huo wa marehemu ulikutwa ndani ya choo cha shimo kinachomilikiwa na Festo Sigala ambaye kwa sasa ni marehemu
Amesema baada ya hapo wananchi waliamua kumsaka mtuhumiwa huyo ambapo walimkuta eneo la stendi ya mabasi katika kijiji jirani cha Tandala wakati akijaribu kutoroka baada ya kupata taarifa kuwa wamegundua kama alifanya mauaji, na wakaanza kumpa kipigo
"Walimkuta stendi huyo mtuhumiwa akiwa anataka kutoroka baada ya kujua kuwa anatuhumiwa kwa mauaji na mwili wa marehemu ulikutwa kwenye choo chake na wakaanza kumpiga kwa mawe, fimbo wakati alipotaka kutoroka eneo hilo" alisema Kasonde
Kufuatia kipigo cha wananchi hao kuwa kikali, mtuhumiwa huyo aliamua kutimua mbio kuelekea kituo cha polisi Tandala kwa lengo la kujisalimisha, lakini wananchi hao waliendelea kumfukuza na wakafanikiwa kumzingira na kuendelea kumshambulia kwa kipigo hasa maeneo ya kichwani amapo ubongo na damu vilimwagika kwa vingi hadi alipofariki dunia kabla hajafika kwenye kituo cha polisi
Amesema kutokana na wingi wa wananchi hao walioamua kujichukulia sheria mkononi, polisi waliokuwa kazini katika kituo hicho walizidiwa nguvu na kundi hilo la watu hivyo kushindwa kumnusuru mtuhumiwa huyo asiuawe kwani nguvu ya wananchi ilikuwa ni kubwa
hata hivyo baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa marehemu huyo aliuawa akiwa ndani ya kituo hicho cha Polisi baada ya wananchi kuwazidi nguvu polisi na kuvinja chumba alichokuwepo marehemu, lakini suala hilo limekanushwa na OCD Kasonde na kusema kuwa kituo hicho kipo salama na wala marehemu hakuuawa kwenye kituo cha polisi
"Hakuna ukweli wowote wa taarifa kuwa ameuawa akiwa lokapu ya kituo cha polisi Tandala, hakuna kituo kilichovunjwa na badala yake wananchi wenye hasira kali ndio waliomuua wakati akikimbilia polisi kunusuru maisha yake" alisema OCD Kasonde
Katika hatua nyingine ameiomba jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani ni kosa kisheria na badala yake wakimkamata mtuhumiwa wanatakiwa kumfikisha polisi ili sheria ichukuliwe
hadi sasa hakuna anayeshikiliwa kuhusiana na mauaji hayo na uchunguzi bado unaendelea
UTAFITI WAONESHA KIFUA KIKUU(TB) KUSUMBUA VIJIJINI ZAIDI UKILINGANISHA NA MIJINI
Posted on 12:52 by Unknown
Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele nchini.Dr Upendo Mwingira akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika mkutano wa Kimataifa cha taasisi za afya za jamii unaofanyika mkoani Arusha.
Wataalamu wakifuatilia mada zilizokua zikiwasilishwa na mabingwa wa tafiti za magonjwa ya binadamu leo.
Dar lauded for KILIMO KWANZA (Agriculture First) Initiatives
Posted on 12:50 by Unknown
United States journalists who had paid a courtesy visit to the Honorable Minister Eng. Christopher Chiza. The 15 US journalists are in the country from September 29 to October 9, 2013 through the John Hopkins International Reporting Project, funded by the Bill and Melinda Gates Foundation. The Bill and Melinda Gates Foundation had been devoting most of its time and resources to support any efforts aimed at transforming Africa from poverty eradication through its agriculture sector.
Listening on is Dr. Mary Shetto, Head of the Interim Ministerial Delivery Unit under Big Results Now Initiative. Dr. Shetto is also the Coordinator for SAGCOT.
Also in attendance is Mr. Frank Mhina (left), Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs, Mr. Job Mika (center), Private Assistant to Hon. Eng. Chiza and Mr. Erick Kabendera, Freelance Journalist.
Hon. Eng. Christopher Chiza (MP), Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives explains about SAGCOT and Kilimo Kwanza initiatives.
Part of the US team of journalists during the meeting.
By TAGIE DAISY MWAKAWAGO
The Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives, Eng. Christopher Chiza (MP), said that Tanzania is first an agricultural-country, placing Southern corridor strategically as a starting point in yielding resources for the country’s economy.
The Minister said earlier today when he was speaking with the 15 journalists from the United States of America, who are in the country to learn more about agriculture sector and food security initiatives.
The journalists have selected Tanzania for an in-depth fact-finding mission because of its notable record on agriculture, food security and scaling-up nutrition initiatives. “We want to learn more about the success of SAGCOT and Kilimo Kwanza,” said Ms. Alexandra Frank, Project Manager from the John Hopkins University, where the group is enrolled in an International Reporting Project (IRP) in Washington DC.
During their discussion, Hon. Eng. Chiza said that the country is blessed with water resources, but still needs a contribution of about 25 percent of agricultural irrigation to self-sustain its economy.
“Our Government has initiated Big Results Now (BRN) which targets an increase of over 100,000 tons of maize and 250,000 tons of sugar and 190,000 tons of rice, all to be added to the national basket through combination of irrigation and improvement of agricultural marketing systems in the coming two years,” said the Minister.
When posed with question about Kilimo Kwanza and how Tanzania has been able to materialize on agriculture sector, Eng. Minister Chiza said that the Government had initiated the Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT), as part of implementing Kilimo Kwanza initiative which encompasses broader aspect of green revolution and economic development of the country.
“We are trying to bring in large scale farmers to co-exist with the small scale farmers,” said Minister Chiza, adding that the Government wants the SAGCOT model to be the future replica for other corridors in the countries. The current Southern corridor includes Mbeya, Iringa, Njombe, Dar es Salaam, Morogoro, Coast, Rukwa and Ruvuma Region.
The Minister further said that the country’s investment targets its own agriculture production and productivity, and as such, the Government has allocated 10 percent of its National Budget to the agriculture sector, however, its current allocation figure surges steadily at an 8 percent, noted the Minister. The allocation derived from the implementation of the Maputo Declaration which was reached by the heads of state and government of the African Union (AU) at its second ordinary session held between July 10 and 12, 2013 whereby member-states agreed to allocate at least 10 percent of their national budgetary resources to agriculture.
Discussing the success story of the Kilombero rice plantation in Morogoro, Minister Chiza cited statistics of maize production which had increased for some smallholder farmers from 1.5 to 4.5 tons per hectare, while the yields for rice have increased from 2.5 to 6.5 tons per hectare in the target areas.
As for young generation, Minister Chiza said that the Government has put in place a Youth in Agriculture program, which targets young people who are “capable, marketable and have a conducive atmosphere set for them to get employment or employ themselves”. He however acknowledges the need for more investment in science and technology in order to increase farm machineries. “Currently, there is about 70 percent of farmers are still using hand hoe tools and about 64 percent of farmers using tractors,” said the Minister.
In addressing the climate change issue, the Minister said that Tanzania is taking all necessary measures within its capacity in making sure to put in place mitigation and adaptation measures to address challenges brought about by climate change. Tanzania rests on a 945,000 square kilometres and that the rain is therefore limited. “Our goal is to produce more crops suitable for rainy seasons and crops that are drought resistible,” explained Hon. Eng. Chiza.
“Taste can be an issue to some farmers as they tend to grow more maize rather than finding alternative crops to grow that can likely be sustainable and resistible to the particular seasonal-weather,” said the Minister.
The Minister further explained that there is also a need to improve transport network and educate farmers about agro ecological zones and green revolution. “We need long term measures that can address permanent maintenance strategy in order to improve transport network, increase fertilizer use per hectare currently at an 8 kilogram to about 11 kilograms per hectare,” he explained.
The 15 US journalists are in the country from September 29 to October 9, 2013 through the John Hopkins International Reporting Project, funded by the Bill and Melinda Gates Foundation. The Bill and Melinda Gates Foundation had been devoting most of its time and resources to support any efforts aimed at transforming Africa from poverty eradication through its agriculture sector.
The group is expected to wrap up its tour by visiting the KINU Innovation Space in Dar es Salaam, the iAGRI Project at Sokoine University in Morogoro, the One Acre Fund in Iringa and the Oikos East Africa group in Arusha, before returning back to the United States on October 9, 2013.
PEMBE ZA NDOVU, UGAIDI NI VITA YA KIMATAIFA: KIKWETE
Posted on 12:27 by Unknown
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema ujangili wa pembe za ndovu na faru ni tatizo la kimataifa linaolohitaji kutokomezwa kwa ushirikiano huku akitaka mataifa makubwa kudhibiti soko la pembe hizo, hatua ambayo amesema inaweza kukomesha uwindaji haramu unaoathiri utalii barani Afrika.
Katika mahojiano amaaluma na Joseph Msami wa idhaa ya Kiswahili ya radio ya Umoja wa Mataifa mjini New York, rais Kikwete ambaye pia ameelezea hatari ya ugaidi nchini mwake na duniani kwa ujumla amesema hata hivyo nchi yake imechukua tahadhari kujihami na mashambulizi hayo. Kwanza Rais Kikwete anaanza kufafanua ukubwa wa tataizo la uwindaji wa pembe za ndovu na faru.
President Obama Delivers a Statement on the Government Shutdown
Posted on 12:12 by Unknown
By The White House In the Rose Garden at the White House, President Obama delivers a statement to the press on the Affordable Care Act and the Government Shutdown. October 1, 2013.
Lindi na Mtwara wapata washirika kutoka Norway
Posted on 09:04 by Unknown
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Meya wa mji wa Hammerfest ulioko Norway, Alf Jakobsen. Waziri aliongoza Ujumbe kutoka Tanzania katika ziara ya mafunzo nchini Norway hivi karibuni, kuhusu namna ambavyo sekta ya gesi inaweza kutumika kukuza uchumi wa nchi.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisalimiana na Meya wa mji wa Sandnessjoen nchini Norway, Bard Anders alipofika ofisini kwake kwa mazungumzo. Waziri na Ujumbe kutoka Tanzania walitembelea nchini humo hivi karibuni kwa ziara ya mafunzo kuhusiana na gesi asilia.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (mwenye koti refu) akijadiliana jambo na Meya wa mji wa Sandnessjoen, Bard Anders (kulia kwa Waziri) na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ingunn Klepsvik (wa kwanza kushoto.) Waziri Muhongo na Ujumbe wake walikuwa katika ziara ya mafunzo ya gesi asilia nchini Norway hivi karibuni.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (mstari wa mbele-katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe ulioongozana naye katika ziara ya mafunzo kuhusu gesi asilia nchini Norway, pamoja na wenyeji wao mjini Sandnessjoen.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
President Kikwete congratulates Nigeria on achieving 53 years of independence
Posted on 08:34 by Unknown
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a Congratulatory Message to H.E. Dr. Goodluck Jonathan, President of the Federal Republic of Nigeria on the occasion of celebrating the 53rd anniversary of the independence of the Federal Republic of Nigeria on the 1st of October, 2013.
The message reads as follows:
“His Excellency Dr. Goodluck Jonathan
President of the Federal Republic of Nigeria
ABUJA
Your Excellency and Dear Brother,
On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania and, indeed on my own behalf, I would like to extend to Your Excellency and through you to the Government and People of the Federal Republic of Nigeria, our heartfelt congratulations on the occasion of celebrating the 53rd anniversary of the independence of the Federal Republic of Nigeria.
As we join you in celebrating this historic occasion, we note with satisfaction that our two countries continue to enjoy cordial relations. In this connection, I wish to reiterate my desire as well as that of the Government and People of the United Republic of Tanzania to further enhance and strengthen the cordial relations that so happily exist between our two countries by exploring more opportunities of cooperation for the mutual benefit of our peoples.
Please accept, Your Excellency and Dear Brother, my personal best wishes for your continued good health and for the progress and prosperity of the People of the Federal Republic of Nigeria.
Jakaya Mrisho Kikwete
PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA”
Issued by:
The Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation,
Dar es Salaam,
1st October, 2013.
Mvua yakata barabara kijiji cha Ndungu Wilayani Same
Posted on 08:27 by Unknown
Wakazi wa Kijiji cha Ndungu Wilayani Same,wakiangalia Greda likiendelea na kazi ya kusawazisha njia mara baada ya kumomonyoka kwa udongo katika eneo linalojengwa Daraja na kupelekea magari kushindwa kupita kwa muda.hali hiyo imekuja kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha Wilayani humo.zoezi hili lilichukua takribani saa moja na nusu na kufanikiwa kupita kwa magari yaliyokuwa yamekwama kupisha zoezi hilo.
Sehemu iliyomomonjoka kutokana na wingi wa maji ya mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa.
Kazi ikiendelea.
Baadhi ya magari na pikipiki yakiwa yamesimama kupisha zoezi la usawazishaji wa njia.
Magari yalianza kupita japo ilikuwa ni kwa shida.
KONGAMANO LA JUMUIYA YA WAZEE WASTAAFU,WAKULIMA NA WAFANYAKAZI LAFANYIKA ZANZIBAR
Posted on 07:57 by Unknown
Mwenyekiti wa Kongamano la Jumuiya ya wazee wastaafu,walimu na wafanyakazi Ali Hassan Khamiss akielezea mada ya umuhimu wa historia katika nchi kushoto ni Salum Maalim Salum ni Mjumbe wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utamadunu, Utalii na Michezo Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Mmoja kati ya wazee Ali Juma Chum kutoka Shehia ya Magogoni Mjini Unguja akichangia katika Kongamano la Jumuiya wazee, wastaaafu,wakulima na wafanyakazi huko ukumbi wa Wizara ya Habari Utamadunu Utalii na Michezo Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Mmoja wa wazee Haji Seti Haji kutoka Shehiya ya Mpendae Mjini Unguja akichangia umuhimu wa historiya ya Zanzibar na utamaduni wake ulindwe na kuezniwa ili usije ukatoweka huko ukumbi wa Wizara ya Habari Utamadunu Utalii na Michezo Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Wazee ,wastaafu ,walimu na wafanya kazi wakisikiliza maeelezo katika Kongamano la Jumuiya wazee, wastaaafu, wakulima na wafayakazi katika ukumbi wa Wizara ya Habari,Utamadunu, Utalii na Michezo Kikwajuni Mjini Zanzibar. (Picha na Miza Othmani Maelezo-Zanzibar).
Rais Dk.Shein akutana na Balozi wa Uholanzi na Balozi Mdogo wa China.
Posted on 06:36 by Unknown
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Uholanzi Nchini
Tanzania Jaap Frederiks,alipofika leo Ikulu Mjini Zanzibar kwa
madhumuni ya kusalimiana na Rais.
Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Uholanzi Nchini
Tanzania Jaap Frederiks,alipofika leo Ikulu Mjini Zanzibar kwa
madhumuni ya kusalimiana na Rais.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Uholanzi Nchini
Tanzania Jaap Frederiks, alipofika leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Uholanzi Nchini
Tanzania Jaap Frederiks, alipofika leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akiagana na Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania
Jaap Frederiks,baada ya mazungumzo yao,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar
leo.
Dk.Ali Mohamed Shein,akiagana na Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania
Jaap Frederiks,baada ya mazungumzo yao,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar
leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi Mdogo wa China Nchini
Tanzania ,anayefanyia kazi zake Zanzibar Xie Yunliang,alipofika jana
Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi Mdogo wa China Nchini
Tanzania ,anayefanyia kazi zake Zanzibar Xie Yunliang,alipofika jana
Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi Mdogo wa China Nchini
Tanzania,anayefanyia kazi Zanzibar Xie Yunliang, alipofika jana Ikulu
Mjini Zanzibar leo.
Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi Mdogo wa China Nchini
Tanzania,anayefanyia kazi Zanzibar Xie Yunliang, alipofika jana Ikulu
Mjini Zanzibar leo.
Balozi wa Marekani aiaga Wizara ya Mambo Ndani ya Nchi
Posted on 06:11 by Unknown
Balozi wa Marekani Nchini, Alfonso E. Lenhardt leo Agosti Mosi, 2013, amezuru Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kuiaga Menejimenti ya Wizara.
Akizungumza na Menejimenti amesema idara za Wizara hiyo ambazo ni pamoja na Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto, Wakimbizi, Huduma kwa Jamii na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa zinafanya kazi nzuri ya kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.
Amesema yeye na familia yake kamwe hawataisahau Tanzania kwa sababu walipata makaribisho mazuri na wameishi kwa amani na huku kukiwa na ushirikiano mzuri kutoka kwenye vyombo vya usalama.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi amemshukuru Balozi Lenhardt kwa ushirikiano na mchango mkubwa wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo chini ya Wizara hiyo na idara zake aliokuwa akitoa kutoka nchini mwake.
Amesema ana amini Balozi ajaye atakuwa na ushirikiano mzuri na Wizara yake na Serikali kwa ujumla.
Akizungumza na Menejimenti amesema idara za Wizara hiyo ambazo ni pamoja na Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto, Wakimbizi, Huduma kwa Jamii na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa zinafanya kazi nzuri ya kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.
Amesema yeye na familia yake kamwe hawataisahau Tanzania kwa sababu walipata makaribisho mazuri na wameishi kwa amani na huku kukiwa na ushirikiano mzuri kutoka kwenye vyombo vya usalama.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi amemshukuru Balozi Lenhardt kwa ushirikiano na mchango mkubwa wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo chini ya Wizara hiyo na idara zake aliokuwa akitoa kutoka nchini mwake.
Amesema ana amini Balozi ajaye atakuwa na ushirikiano mzuri na Wizara yake na Serikali kwa ujumla.
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU WAZEE DUNIANI NA WAZEE WA KOROGWE MKOA WA TANGA.
Posted on 06:03 by Unknown
Akivishwa vazi la Asili la
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Wazee waliohudhuria katika sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, baada ya kuhutubia katika sherehe hizo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Mandu, Korogwe Mkoani Tanga leo Okt. 01, 2013. Picha na OMR.
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAWATAHADHARISHA WAKULIMA WAKE WA VIJIJI
Posted on 04:56 by Unknown
Mmoja kati ya Wakulima wa Kijiji cha Nguruweni Dole Mzee Kitwana Mustaha aliishukuru na Kuipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa kukamilisha ahadi yake ya kuwapatia hati za umiliki wa mashamba wakulima hao kwa ajili ya kilimo katika maeneo yaliyowahi kuleta mgogoro kwa muda mrefu.
Baadhi ya wananchi na wakulima wa Kijiji cha Nguruweni wakiwa katika mkutano maalum uliotishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif wa kukabidhiwa hati za umiliki wa mashamba ya kilimo katika maeneo yao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Nguruweni kabla ya kuwakabidhi hati za umiliki wa mashamba ya kilimo wakulima hao.
Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi Hati ya umiliki wa shamba Bibi Josephine Yohana kwenye hafla maalum ya kumaliza mgogoro wa mashamba katika kijiji hicho.
Balozi Seif akimpatia Hati Bwana Mohd Ali Pili ya kumiliki eneo la kilimo katika Kijiji cha Nguruweni ambako kuliibuka mgogoro uliosababishwa na kuinbgizwa watu wasiohusika na maeneo hayo kwa kilimo. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
TAARIFA MBALIMBALI ZA MICHEZO KUTOKA KWA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
Posted on 04:31 by Unknown
MECHI ZA YANGA, SIMBA ZAINGIZA MIL 182/-
Mechi za Yanga na Simba za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zilizochezwa wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam zimeingiza jumla ya sh. 182,103,000.
Yanga katika mechi yake dhidi ya Ruvu Shooting iliyochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 imeingiza sh. 94,202,000.
Watazamaji 16,492 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo ambapo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 22,630,921.58. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000, na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 14,369,796.61.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 11,507,248.26, tiketi sh. 3,117,215, gharama za mechi sh. 6,904,348.96, Kamati ya Ligi sh. 6,904,348.96, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,452,174.48 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,685,024.59.
Nayo Simba ambayo iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu katika mechi iliyochezwa Jumapili (Septemba 29 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 87,901,000.
Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 41 walikuwa 15,780. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 21,051,025.92 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 13,408,627.12.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 10,703,911.48, tiketi sh. 3,132,963, gharama za mechi sh. 6,422,346.89, Kamati ya Ligi sh. 6,422,346.89, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,211,173.44, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,248,789.67 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 1,248,789.67.
Wakati huo huo, mechi ya ligi hiyo kati ya Mbeya City na Coastal Union iliyochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya imeingiza sh. 16,959,000 huku kila klabu ikipata sh. 4,035,229.
Mgawo wa mechi hiyo ulikuwa ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 2,586,966, uwanja sh. 2,051,811.57, tiketi sh. 696,290, gharama za mechi sh. 1,231,086, Kamati ya Ligi sh. 1,231,086, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 615,543, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA) sh. 478,756.
MICHUANO YA CHALENJI KUANZA NOV 27
Michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) inafanyika Kenya kuanzia Novemba 27 hadi Desemba 12 mwaka huu.
Nchi wanachama ambazo zinataka kushiriki zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kwa Sekretarieti ya CECAFA kabla ya Oktoba 20 mwaka huu. Wanachama wa CECAFA ni Burundi, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania, Uganda na Zanzibar.
Michuano hiyo itatanguliwa na Mkutano Mkuu wa CECAFA utakaofanyika Novemba 26 mwaka huu ambao pamoja na mambo mengine utakuwa na ajenda ya uchaguzi. Uchaguzi huo ni kwa ajili ya kujaza nafasi nne za wajumbe wa Kamati ya Utendaji.
Wajumbe wanaomaliza muda wao ni Sahilu Gebremarian wa Ethiopia ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CECAFA, Abdigaani Saed Arab (Somalia), Tariq Atta (Sudan) na Raoul Gisanura (Rwanda).
Majina ya wagombea yanatakiwa kuwa yamewasilishwa katika Sekretarieti ya CECAFA kabla ya Oktoba 20 mwaka huu, na yakiwa yamethibitishwa na vyama vyao vya mpira wa miguu.
SUALA LA PAPIC, YANGA LASUBIRI UAMUZI WA FIFA
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limewasilisha rasmi suala la madai ya aliyekuwa Kocha wa Yanga, Kostadin Papic dhidi ya klabu hiyo katika Kamati ya Hadhi ya Wachezaji.
FIFA imesema imepeleka rasmi suala hilo katika kamati yake hiyo baada ya kupokea vielelezo vya Papic anayedai kuidai Yanga dola 10,000 za Marekani pamoja na vile vya Yanga inayodai kumlipa kocha huyo fedha zote alizokuwa akiidai klabu hiyo.
Kwa taratibu za FIFA, hivi sasa haitapokea vielelezo vingine kutoka pande hizo mbili, na badala yake Kamati hiyo inayoongozwa na Theo Zwanziger kutoka Ujerumani itafanya uamuzi na kuziarifu pande husika. Zwanziger kitaaluma ni mwanasheria.
Papic aliyeinoa Yanga kwa vipindi viwili tofauti aliwasilisha malalamiko yake FIFA akidai hadi mkataba wake unamalizika klabu hiyo ilikuwa haijamlipa dola 10,000 za Marekani.
LIPULI, MAJIMAJI KUUMANA WAMBI FDL.
Mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Lipuli ya Iringa na Majimaji ya Songea sasa itachezwa kesho (Oktoba 2 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Wambi uliopo Mafinga badala ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.
Mabadiliko hayo yamefanyika kutokana na Serikali kuutumia Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora kwa ajili ya shughuli za mbio za Mwenge.
Mechi nyingine ya FDL kesho itakuwa kati ya Tessema FC ya Dar es Salaam na Ndanda FC ya Mtwara, na itafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
MAALIM SEIF AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WALIMU ZANZIBAR
Posted on 02:54 by Unknown
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na viongozi wa Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), Ofisini kwake Migombani.
Rais wa Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), Salim Kitwana Sururu (kushoto), akiwasilisha maoni ya chama hicho kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Ofisini kwake Migombani.
Rais wa Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), Salim Kitwana Sururu (kushoto), akiwasilisha maoni ya chama hicho kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Ofisini kwake Migombani.
Baadhi ya viongozi wa Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), walimsikiliza Maalim Seif, walipokutana nae Ofisini kwake Migombani. (Picha na Salmin Said, OMKR).
===== ======= =========
Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), kimepongezwa kutokana na uvumilivu walionao katika kutafuta njia muafaka za kutatua kero zinazowakabili.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, ametoa pongezi hizo Ofisini kwake Migombani, wakati akizungumza na viongozi wa Chama hicho wakiongozwa na Rais wa ZATU, Salim Kitwana Sururu.
Amesema takriban nchi zote za Afrika Mashariki zimekuwa zikikumbwa na migogoro kati ya serikali na vyama vya walimu, lakini ni jambo la kufurahisha kuona Chama Cha Walimu Zanzibar hakiingi katika migogoro hiyo na badala yake kimekuwa kikitumia njia za Kidiplomasia katika kutatua kero zake.
Amekitaka Chama hicho kuendeleza moyo huo, kwani njia bora ya kutatua mizozo ni mazungumzo, na wala sio malumbano au migomo.
Amefahamisha kuwa uzoefu unaonesha kuwa mara nyingi inapotokea migomo ya walimu linaloathirika ni Taifa na vijana, na kwamba hakuna haja ya kushiriki au kushabikia malumbano ya aina hiyo.
Ameeleza kuwa Serikali kwa upande wake iko tayari kukutana na wadau mbali mbali kujadiliana juu ya kero zinazowakabili, ili kutafuta njia ya kuzitatua kwa njia ya amani bila ya kuwepo malumbano.“Hakuna lisilozungumzika, na mimi nasema njia muafaka ya kutatua kero za namna hiyo ni mazungumzo. Kwa hivyo endeleeni na moyo huo huo na bila ya shaka kero zenu zitatatuka”, alisema Maalim Seif kuwambia wakuu wa ZATU.
Kwa upande wake Rais wa Chama Cha Walimu Zanzibar (ZATU), Salim Kitwana Sururu, amesema ni heshima kubwa kwa Zanzibar kutokumbwa na migomo ya walimu ambayo imekuwa ikijitokeza katika nchi jirani mara kwa mara.Ameahidi kuwa ZATU kitaendelea kutumia njia za mazungumzo katika kutatua kero zinazowakabili, na kwamba kitafanya hivyo ili kulinda heshima ya Zanzibar.
Naye Katibu Mkuu wa Chama hicho Mussa Omar Tafurwa, ameiomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kuitekeleza kikamilifu Sera ya Elimu Zanzibar, ili kuleta maendeleo yaliyokusudiwa katika sekta ya elimu.
Amefahamisha kuwa bado yapo mambo mengi ambayo hayajatekelezwa ndani ya sera ya elimu ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Mamlaka ya uajiri wa walimu, pamoja na Baraza la Walimu Zanzibar, mambo ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi.
Subscribe to:
Posts (Atom)