Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesisitiza kuwa kitaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaotaka kuwekeza katika mikoa ya kanda ya kaskazini na maeneo mengine nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kongamano la uwekezaji kanda ya kaskazini lililomalizika hivi karibuni mjini Tanga, Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Bi. Juliet Kairuki alisema kuwa kituo chake kiko tayari kupokea wale wote walio tayari kuwekeza katika kanda hiyo.
“Kwa wale ambao watakuwa tayari kuwekeza katika mikoa ya kanda ya kaskazini, milango ipo wazi kuandikisha miradi yao TIC,” alisema mjini Tanga hivi karibuni.
Akielezea kongamano hilo ambalo ni la kwanza kufanyika katika kanda hiyo alisema huo ni mwanzo wa juhudi kama hizo katika kutangaza vivutio vya uwekezaji katika kanda hiyo na maeneo mengine ya nchi.
0 comments:
Post a Comment