50 Bing Coupons

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 22 September 2013

OPERESHENI KIMBUNGA AWAMU YA KWANZA YAFIKIA KILELE KWA MAFANIKIO

Posted on 03:05 by Unknown
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI




Operesheni Kimbunga iliyoanza Septemba 6,2013 imemaliza utekelezaji wa Awamu yake ya Kwanza Septemba 20, 2013 kwa kutimiza malengo yake kwa mafanikio makubwa.
Hadi kufikia mwisho wa Awamu ya Kwanza wa Operesheni hii, Timu ya Operesheni imefanikiwa kukamata wahalifu wa unyang’anyi wa kutumia silaha pamoja na washirika wao na kuhakiki uraia wa watuhumiwa wa Uhamiaji haramu kwa kutumia maofisa wa Idara ya Uhamiaji kwa kuzingatia Sheria za Uhamiaji. Aidha, suala la Haki za Binaadam limezingatiwa katika Operesheni hii.
Jumla ya Wahamiaji haramu 12,704 wamekamatwa, kati yao Wanyarwanda 3,448 Warundi 6,125, Waganda 2,496, Wakongo 589 Wasomali 44, Yemen 1 na India 1.
Jumla ya Wahamiaji Haramu 194 walirudishwa na kupokelewa nchini baada ya kukataliwa na nchi zao. Watu hao wanasubiri  hatua za kisheria kuchukuliwa kwa kuwa hawana sifa ya kuwa Raia wa Tanzania na pia wamekosa sifa ya kuwa raia wa nchi jirani ambapo Serikali iliwapeleka baada ya vigezo vya kuthibitisha kuwa ni raia wa nchi hizo kukamilika.
Wakati Operesheni kimbunga inafanyika katika Awamu yake ya Kwanza kuanzia Septemba 6, 2013, jumla ya wahamiaji haramu 2,129 walikubali kuondoka nchini kwa hiari yao na Wahamiaji Haramu  8,696 waliondoshwa nchini kwa amri ya Mahakama baada ya kupewa hati ya kufukuzwa nchini. Watuhumiwa wa Uhamiaji Haramu 1,852 waliachiwa huru baada ya Serikali kuthibitisha uraia wao wakati wengine 2,286 wanaendelea na mahojiano ili kuthibitisha uraia wao. 
Operesheni Kimbunga pamoja na kushughulikia wahamiaji Haramu ilifanikiwa kukamata jumla ya Watuhumiwa 212 wa unyang’anyi wa kutumia silaha na Majangili wa Tanzania 23. Mabomu 10 ya kutupwa kwa mkono, bunduki/silaha 61 zikiwemo bunduki aina ya SMG 5, Shot Gun 8, Mark IV 1, Riffle 1, Pistol 1, Pisto za kienyeji 3 na Magobole 42 pamoja na mitambo Miwili 2 ya kutengeneza silaha aina ya Magobole.
Risasi 665 zilikamatwa zikiwemo za bunduki aina ya SMG na SAR risasi 561, Shot Gun risasi 22, Gobole risasi 82 na Fataki 8, Suruali Sare za Jeshi na Kibuyu cha Maji vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
Jumla ya Ng’ombe 8,226 walikamatwa wakiwa wanachungwa katika maeneo ya Tanzania hususan katika hifadhi za misitu. Pia kiasi cha Tsh. 32,510,000/= zimepatikana ikiwa ni tozo za faini ya ng’ombe walioachwa kwenye hifadhi ya Taifa.
Ngozi za wanyama aina ya Duma(1), Swala (2), Nyati (1) na vipande 10 vya Nyama vinavyodhaniwa kuwa Nyara za Serikal, Vipande viwili vya meno ya Tembo pamoja na Mbao 2,105, Magogo 86, Mkaa Magunia 467,Gongo Lita 375, Mtambo wa Gongo mmoja (1), Bangi Kilo 77 na Makokoro yanayotumika kuvuna Samaki kinyume cha sheria  vilikamatwa katika kipindi cha Wiki Mbili za Awamu ya Kwanza ya Operesheni Kimbunga.
Takwimu zinaonyesa kuwa Mkoa wa Kagera unaongoza kwa kukamata wahamiaji haramu 7,001 ukifuatiwa na Mkoa wa Kigoma ambaPo wahamiaji haramu 5,005 walikamatwa wakati mkoa wa Geita wamekatwa Wahamiaji Haramu 698.
Changamoto
Pamoja na mafanikio yaliyopatikana kumekuwepo na changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na hali ya maisha mchanganyiko ya Watanzania asilimia 60% na Wahamiaji asilimia 40% katika mikoa ya mpakani hii ni kwa mujibu wa tafiti mbali mbali za masuala ya kiuhamiaji zilizowahi kufanyika katika mikoa hiyo.
Changamoto nyingine ni baadhi ya wananchi wenye nia mbaya au kulipizana visasi walitaka kutumia zoezi hili kuweza kukomoana kwa kuwataja baadhi ya watu kuwa ni wahalifu kumbe ni uongo na baadhi ya wahamiaji baada ya kukamatwa walikosa sifa za uraia wa Tanzania na hata waliporudishwa kwenye nchi wanazodhaniwa kutoka walikosa sifa za uraia na kuleta mgongano kuhusiana na uraia wao yaani kwa kiingereza (Stateless citizenship) .
Changamoto nyingine zilizojitokeza ni pamoja na ukosefu wa Vitambulisho vya Uraia (Utaifa) ambako kulileta tatizo katika kuwatambua Wahamiaji Haramu na kutokuwepo kwa uzio wa kuzuia mipaka ya nchi yetu hivyo Wahamiaji Haramu wanapopelekwa kwao wanarudi kupitia vipenyo visivyo halali yaani njia za panya.
Sheria ya Maliasili na Utalii (The Forest Act & Wild Life Conservation Act) kutoendana na hali halisi ya uhalifu wa uhujumu wa Maliasilia, mfano kifungu cha 81 (2) kinatoa adhabu ya faini kuanzia shilingi Elfu Thelathini (30,000/=) hadi Milioni Moja na uzoefu unaonyesha kwamba wanaotenda makosa hayo hupigwa faini chini ya Shilingi Laki Tano (500,000/=) bila kujali thamani ya mali aliyokamatwa nayo, isipokuwa maamuzi hutegemea utashi wa Mahakama.
Matarajio
Baada ya kukamilisha Awamu ya Kwanza ya Operesheni Kimbunga tunatarajia Serikali kushughulikia changamoto zilizojitokeza ili kupunguza baadhi ya matatizo katika mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita hususan yanayohusia na uhalifu na masuala ya kiuhamiaji.
Tunatarajia kuanzisha kikosi kazi kila mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa wahalifu sugu wanaotumia silaha za kivita na wale wanaowafadhili.
Aidha, uhamasishaji utafanyika kuanzia ngazi ya familia, Kitongoji, Mtaa/Kijiji, Kata/Shehia, Tarafa, Wilaya Mkoa na Taifa kuhamsisha jamii kuimarisha misingi ya ulinzi na usalama kupitia kwenye kamati zilizopo na kutoa taarifa mara moja pindi panapojitokeza jambo lolote linalohusu ulinzi na usalama katika maeneo yao.
Aidha, tunatarajia kujipanga kimkakati ili kuona namna ya kushughulikia baadhi ya Wahamiaji Haramu waliokosa sifa za uraia na kurudishwa nchini mwao ambao bado wanang’ang’ania kwa kusema wao ni Watanzania (stateless citizenship).
                                                          
                                                                  Washiriki                     
Operesheni Kimbunga ilishirikisha Vyombo Vya Ulinzi na Usalama wakiwemo Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi, Usalama wa Taifa, Uhamiaji, Magereza, TAKUKURU, Taasisi nyingine za Serikali zikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na  Idara za Mifugo,  Ardhi, Kilimo, Uvuvi, Misitu, Afya na Idara ya Wanyama Pori.
Hitimisho
Opereshi Kimbunga ilifanyika kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi. Aidha, suala la Haki za Binaadam lilizingatiwa na hadi sasa hakuna malalamiko yeyote yaliyopokelewa.
 Hata hivyo, juhudi na nguvu zaidi zitaelekezwa katika kukamata Majambazi, Silaha Haramu, Majangili na Wahamiaji Haramu. 
Mafanikio yaliyofikiwa yametokana na ushirikiano wa Maofisa Wakuu Waandamizi, Maofisa wa Kati, Wakaguzi na Askari wote wa vyeo mbali mbali walioshiriki kwenye utekelezaji wa operesheni hii. Kila mtendaji alitimiza wajibu na majukumu yake na ndiyo maana malengo ya utekelezaji wa operesheni hii yamefikwa kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo huu ni mwisho wa Awamu ya Kwanza ya operesheni na mwanzo wa Awamu ya Pili ya Operesheni Kimbunga kwa maana nyingine Operesheni inaendelea mpaka hapo hali ya usalama ya mikoa hii Mitatu itakapokuwa shwari.

 Taarifa hii imetolewa na:
Naibu Kamishna wa Polisi Simon Sirro 
kwa niaba ya Kamanda wa Operesheni Kimbunga 
Mwanza, Septemba22,2013


Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • tamasha la 32 la sanaa la bagamoyo lawasha moto, Mhe Makala asema utamaduni ni ajira kwa vijana
    NAIBU Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makala amesema Sanaa na Utamaduni nchini itaendelea kuenziwa ili kuwaleta a...
  • WAZIRI DK. NCHIMBI AMTEMBELEA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI HOSPITALI YA MUHIMBILI LEO
    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Pa...
  • wadau farida na paul wameremeta
     Wakila pozi baada ya kumeremeta katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam kabla ya kwenda kwenye mnuso wao wa nguvu katika hote...
  • RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU YA CHUO KIKUU CHA GUELPH JIMBONI ONTARIO, CANADA
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa ...
  • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHINGTON, DC YAFANA
    Katibu wa Jumuiya ya Tanzania akielezea nini maana ya GLN na kwanini Jumuiya ya Tanzania DMV ni moja ya washiririki  Banda la Tanzania lilki...
  • ACCT members attending Master Builders South Africa Congres 2013
    Basically ACCT members were invited by CIDB Construction Industry Development Board South Africa to attend at 2 days congress here in Joanes...
  • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMANI TANZANIA
     Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akishiriki kuwasha mshumaa kama tendo la kuiangaza nchi ya Tanzania.  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape ...
  • TAARIFA YA MSIBA WA MAMA ROSE HEINRICH SANGIWA MATAJI
    Familia ya Marehemu Chief Shaaban Mtengeti II, inasikitika kutangaza kifo cha shangazi yao mpendwa  Mama Rose Heinrich Sangiwa Mataji, mama ...
  • MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD AWASILI MKOANI RUKWA KUSHIRIKI IJITIMAI YA KIMATAIFA
    Makamu wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya a...
  • Timu ya Taifa ya Pool yaanza kujifua huko Mkoani Morogoro
    Kocha wa Timu ya Taifa, Denis Lungu (kulia) akiwaelekeza jambo wachezaji wa timu ya Taifa ya mchezo wa Pool (Safari National Pool team) wak...

Blog Archive

  • ▼  2013 (500)
    • ►  October (22)
    • ▼  September (478)
      • HIKI HAPA KILIO CHA WANAFUNZI WA UDAKTARI BUGANDO...
      • No title
      • BREKING NYUUZZZZZZ: SERIKALI YA MAREKANI YAFUNGA S...
      • No title
      • NATURAL PRODUCTS FOR your skin
      • SIKU YA UTALII DUNIANI YENYE KAULI MBIU UTALII NA ...
      • President Kikwete sends Congratulatory Message to ...
      • WAKAZI WA KIKUYU KUSINI WAANDAMANA KUPINGA BOMOABO...
      • ngoma azipendazo ankal
      • wadau farida na paul wameremeta
      • ACCT members attend Master Builders South Africa C...
      • magari yanauzwa
      • Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali Bw L...
      • Spika Makinda apongeza Mabunge ya Afrika kwa kuong...
      • KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA JOHN CASMIR MINJA AH...
      • dk shein aagana na balozi wa marekani aliyemaliza ...
      • KATIBU MKUU UTUMISHI, Bw. GEORGE YAMBESI AFUNGUA M...
      • Maalim Seif aifunga rasmi Ijtimai ya Kimataifa ili...
      • HOJA YA HAJA: TUIENZI AMANI YETU KWA GHARAMA YOYOT...
      • MWIGULU NCHEMBA KUNDURUMA NDANI YA LONDON UINGEREZA
      • mwenge wa uhuru watua jijini mbeya
      • MBUNGE WA VITI MAALUMU TABORA,MH MUNDE TAMBWE ADHA...
      • JK arejea nyumbani kutoka Canada na Marekani
      • JK alipohudhuria Mkutano wa Kukabiliana na Ujangil...
      • Globu ya Jamii yakuletea Exclusive Intavyuuu na Re...
      • KANYABOYA LINGINE LAIBUKA DAR,WADAU KAENI CHONJO
      • WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU AIPONGEZA VODA...
      • TIMU YA WIZARA YA AFYA YATINGA ROBO FAINALI - SHIMIWI
      • SAGCOT CEO meets with the US journalists
      • Redd’s Miss Tanzania 2013/14 atembelea TBL leo
      • KONGAMANO LA WAZEE WASTAAFU LAFANYIKA ZANZIBAR
      • ufunguzi Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Taasis...
      • AJALI ZAPUNGUA MKOANI IRINGA
      • MWAKALEBELA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU 13 M...
      • MAALIM SEIF AWATAKA WAISLAM NCHINI KUUNGA NA KUSHI...
      • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMIRI J...
      • Japanese Grant for the Food Security Project for U...
      • ACCT members attending Master Builders South Afric...
      • Awamu ya pili ya chakula cha hisani cha Taasisi ya...
      • MHE. MWIGULU NCHEMBA AWAKUNA WENGI DMV.
      • MWENGE WAZINDUA UJENZI WA OFISI YA KATA TANDALA WI...
      • WAZIRI CHIKAWE ATEMBELEA GEREZA KUU LA ISANGA,MKOA...
      • MKUTANO WA CCM CHWAKA UNGUJA
      • TAARIFA YA MSIBA
      • SingTel Group and Samsung partner to enhance mobil...
      • TIC yawahakikishia wawekezaji ushirikiano zaidi
      • DIAMOND ALIVYOWAKUNA MASHABIKI WAKE NDANI YA GOLD ...
      • KAPOTIVE STAR SINGER-S BUKOBA KUWASHA MOTO JIJINI ...
      • TFDA YAENDESHA KAMPENI YA UTUMIAJI WA VYAKULA VILI...
      • Wakazi wa eneo la hifadhi ya Ngorongoro wapokea ch...
      • AZANIA BANK YACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI SHULE Y...
      • United States 2015 Diversity Visa Program Now Open
      • OPERESHENI KIMBUNGA AWAMU YA PILI YASHIKA KASI KAT...
      • mdau mugassa mwenda ahojiwa na BBC kwa kufurahishw...
      • Airtel yawanoa maafisa waTRA jinsi ya kulipia ada ...
      • NAIBU WAZIRI FEDHA AKAGUA UJENZI WA BARABARA VISIW...
      • 2013 Young Achievers Awards Nomination Open!
      • No title
      • IN LOVING MEMORY of DORA HOSEA TALAWA 1ST ANNIVESSARY
      • ngoma azipendazo ankal
      • TAARIFA YA MSIBA WA MAMA ROSE HEINRICH SANGIWA MATAJI
      • FRANSIC MIYEYUSHO AMTWANGA SADIK MOMBA KWA POINTI
      • Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Wafanyakazi...
      • Mahojiano ya JK na radio ya umoja wa mataifa, New ...
      • J&M Virgo washusha mali mpya
      • Daktari wa Rais Kikwete kupima afya na kuwapa lese...
      • MWENGE WA UHURU WATUA MAKETE
      • Swali la kizushi: Je ni mkono upi unaofaa kuvalia ...
      • No title
      • No title
      • introducing Mchaga na pesa by KiwaStrond ft. Banx
      • bwawa la maini oye! Suarez arudi na kupiga bee kat...
      • HARAMBEE KUCHANGIA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KUS...
      • introducing 'Ni Noma' by Go Getta of the night cra...
      • MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ...
      • Ubalozi wetu zambia na wajisiriamali wa Tanzania w...
      • Grace aikaeli Mbowe na mumewe wafariki kwa ajali ...
      • Simba yaibanjua Ruvu JKT 2-0 leo neshno
      • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMA...
      • ZUMBA KUKWE AMSHINDA HAMADUU MWALIMU KWA KO RAUNDI...
      • TANZIA: Msiba wa Bi ROSE HENRISCH SANGIWA MATAJI
      • Sherehe za kufunga mafunzo katika kikosi cha 842 ...
      • Benki ya posta Tanzania tawi la Songea yaipiga jek...
      • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHING...
      • TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO NI KWELI KWAMBA LIMEPOTE...
      • No title
      • Tanzanian Minister of Defence Meets Governor of So...
      • UPANUZI WA BARABARA YA BENDERA TATU HADI KAMATA KU...
      • MISS UTALII TANZANIA KUTANGAZA NYATI WA AJABU NA ...
      • Cheka unenepe
      • WAFANYAKAZI WA IDARA MBALI MBALI ZA SERIKALI WACHU...
      • Kiwanda cha kuzalisha malighafi za kutengeneza Gil...
      • MAMA SALMA KIKWETE APEWA URAIA WA HIARI WA JIMBO L...
      • MKUTANO WA SIKU TATU WA MAOFISA WA JUU WA JESHI LA...
      • NBC YATENGA SIKU MAALUMU KUWASHUKURU WATEJA WAO
      • Serikali yabariki tamasha la Utamaduni Handeni
      • Matukio zaidi ya Mhe. Rais Kikwete alipolihutubia ...
      • ngoma azipendazo ankal
      • chemsha bongo...
      • cassim mganga akitumbuiza kwenye tamasha la fiesta...
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile