50 Bing Coupons

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Wednesday, 25 September 2013

Vodacom yakabidhi vifaa vitakavyotumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari dar es salaam

Posted on 23:39 by Unknown
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akishirikiana na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa kukagua vifaa vya michezo muda mfupi kabla ya Waziri kukabidhiwa rasmi vifaa hivyo vitakavyotumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari Mkoa wa Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akipokea vifaa vya michezo kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa. Vifaa hivyo vitatumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari Mkoa wa Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Vodacom ilikabidhi jezi za soka seti 12, mipira 40 na kombe kubwa la Mshindi
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akipokea kombe kubwa kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa atakalokabidhiwa mshindi wa kwanza wa mashindano maalum kwa shule za sekondari Mkoa wa Dar es salaam yanayoandaliwa na Wizara.Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo Juliana Yasoda. Vodacom ilikabidhi pia jezi za soka seti 12 na mipira.
---------------------------

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala leo amepokea vifaa vya michezo kutoka Vodacom kwa ajili ya kutumika kwenye mashindano maalum ya sekondari yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao jijini Dar es salaam.
Akipokea vifaa hivyo ambavyo ni jezi seti 12 na mipira 40 pamoja na kombe kwa ajili ya bingwa wa michuano hiyo Waziri Dk Mukangala ameelezea kufurahishwa kwake jinsi ambavyo Vodacom walivyopokea ombi la Wizara la kusaidia mashindano hayo.
Amesema lengo la mashindano hayo ni kuendeleza azima ya serikali ya kutengeneza fursa ya ukuzaji na uendelezaji michezo kwa ngazi za chini kupitia falsafa ya michezo jamii.
“Michezo ni gharama inahitaji fedha nyingi kugharamia vifaa, mafunzo kwa walimu, viwanja na gharama nyengine za uendeshaji ndio maana naipongeza sana Vodacom kwa kukubali ombi letu la kusaidia mashindano haya maalum yatakoyoshirikisha shule 12 za sekondari za Mkoa wa Dar es salaam.”Alisema
“Mashindano haya ni ya majaribio tukiangalia namna ambavyo tunaweza kuwekeza vya kutosha kwenye michezo ngazi ya mashuleni kwa nchi nzima, tutaanza na mchezo wa soka ila mipango ni kupanua wigo kwa kuongeza mpira wa pete na riadha kwa hapo mwakani ikihusiha mikoa mingi zaidi.”Alisema Dk. Mukangala
Waziri Dk. Mukangala amesema Wizara yake inaimani kubwa juu ya mpango huo huku akizitaka jamii kuyapokea na kuyaona kuwa ni sehemu yao ili pamoja na kuyapapa mafanikio bali pia kuwatia moyo watoto wakati wote watakapokuwa waskishiriki.
Amesema kuwa anatambua kuwa mahitaji ni makubwa na kwamba kila shule hapa nchini ingependa kushiriki lakini kwa kuanzia watachagua shule 12 za sekondari kama majaribio huku mipango ikiendelea kuwekwa sawa ili mashindano hayo yawe mapana zaidi kwa hapo mwakani.
“Tuna shule nyingi hapa tu Dar es salaam tumepata wakati mgumu sana kuchagua wawakilishi wa kila Wilaya lakini kwa sasa tunaanza na hizo chache tukiwa na Vodacom na baada ya kumalizika tutafanya tathmini kuona namna ya kuyaongezea wigo wa ushiriki na wa kijiografia.”Alisema Dk. Mukangala
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa amesema Vodacom inatambua umuhimu wa kuwaandaa wachezaji katika ngazi za chini ili kuwa na uhakika wa maendeleo ya michezo nchini.
“Kukubali kwetu kuwa wadhamini kumesukumwa na imani yetu juu ya maendeleo ya michezo nchini tukiamini katika kuwekeza kwa wanafunzi mashuleni, leo tunafuraha kuwa sehemu ya miapngo ya serikali kukamilisha kile ambacho kila mtu anapenda kukiona kikifanyika katika michezo.”Alisema Twissa
“Tumekuwa wadhamini wa Ligi Kuu Vodacom ambayo imekuwa ikipiga hatua kubwa kimaendeleo hasa kwenye eneo la ushindani hivyo ili mafanikio hayo yawe endelevu ni lazima tuwe na misngi mzuri wa kuzalisha wachezaji wenye ubora na viwango na kwamba njia moja ya msingi ni kuwa na mashindano ya ngazi za chini hasa mashuleni”Alisema Twissa
Amesema vifaa walivyovitoa ni sehemu ya Vodacom kuunga mkono juhudi za serikali za kutekeleza mikakati ya uzalishaji, ukuzaji na uendelezaji wa vipaji na kwamba Vodacom inafurahia mpango huo.

Mashindno hayo maalum yataratibiwa na Baraza la Michezo la Taifa – BMT na kwamba utaratibu umewekwa wa kuapat sekondari 12 kutoka Wilaya tatu za Mkoa wa Dar es salaam ambapo kila Wilaya itatoa sekondari  4.
 

Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • tamasha la 32 la sanaa la bagamoyo lawasha moto, Mhe Makala asema utamaduni ni ajira kwa vijana
    NAIBU Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makala amesema Sanaa na Utamaduni nchini itaendelea kuenziwa ili kuwaleta a...
  • WAZIRI DK. NCHIMBI AMTEMBELEA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI HOSPITALI YA MUHIMBILI LEO
    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Pa...
  • wadau farida na paul wameremeta
     Wakila pozi baada ya kumeremeta katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam kabla ya kwenda kwenye mnuso wao wa nguvu katika hote...
  • RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU YA CHUO KIKUU CHA GUELPH JIMBONI ONTARIO, CANADA
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa ...
  • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHINGTON, DC YAFANA
    Katibu wa Jumuiya ya Tanzania akielezea nini maana ya GLN na kwanini Jumuiya ya Tanzania DMV ni moja ya washiririki  Banda la Tanzania lilki...
  • ACCT members attending Master Builders South Africa Congres 2013
    Basically ACCT members were invited by CIDB Construction Industry Development Board South Africa to attend at 2 days congress here in Joanes...
  • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMANI TANZANIA
     Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akishiriki kuwasha mshumaa kama tendo la kuiangaza nchi ya Tanzania.  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape ...
  • TAARIFA YA MSIBA WA MAMA ROSE HEINRICH SANGIWA MATAJI
    Familia ya Marehemu Chief Shaaban Mtengeti II, inasikitika kutangaza kifo cha shangazi yao mpendwa  Mama Rose Heinrich Sangiwa Mataji, mama ...
  • MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD AWASILI MKOANI RUKWA KUSHIRIKI IJITIMAI YA KIMATAIFA
    Makamu wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya a...
  • Timu ya Taifa ya Pool yaanza kujifua huko Mkoani Morogoro
    Kocha wa Timu ya Taifa, Denis Lungu (kulia) akiwaelekeza jambo wachezaji wa timu ya Taifa ya mchezo wa Pool (Safari National Pool team) wak...

Blog Archive

  • ▼  2013 (500)
    • ►  October (22)
    • ▼  September (478)
      • HIKI HAPA KILIO CHA WANAFUNZI WA UDAKTARI BUGANDO...
      • No title
      • BREKING NYUUZZZZZZ: SERIKALI YA MAREKANI YAFUNGA S...
      • No title
      • NATURAL PRODUCTS FOR your skin
      • SIKU YA UTALII DUNIANI YENYE KAULI MBIU UTALII NA ...
      • President Kikwete sends Congratulatory Message to ...
      • WAKAZI WA KIKUYU KUSINI WAANDAMANA KUPINGA BOMOABO...
      • ngoma azipendazo ankal
      • wadau farida na paul wameremeta
      • ACCT members attend Master Builders South Africa C...
      • magari yanauzwa
      • Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali Bw L...
      • Spika Makinda apongeza Mabunge ya Afrika kwa kuong...
      • KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA JOHN CASMIR MINJA AH...
      • dk shein aagana na balozi wa marekani aliyemaliza ...
      • KATIBU MKUU UTUMISHI, Bw. GEORGE YAMBESI AFUNGUA M...
      • Maalim Seif aifunga rasmi Ijtimai ya Kimataifa ili...
      • HOJA YA HAJA: TUIENZI AMANI YETU KWA GHARAMA YOYOT...
      • MWIGULU NCHEMBA KUNDURUMA NDANI YA LONDON UINGEREZA
      • mwenge wa uhuru watua jijini mbeya
      • MBUNGE WA VITI MAALUMU TABORA,MH MUNDE TAMBWE ADHA...
      • JK arejea nyumbani kutoka Canada na Marekani
      • JK alipohudhuria Mkutano wa Kukabiliana na Ujangil...
      • Globu ya Jamii yakuletea Exclusive Intavyuuu na Re...
      • KANYABOYA LINGINE LAIBUKA DAR,WADAU KAENI CHONJO
      • WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU AIPONGEZA VODA...
      • TIMU YA WIZARA YA AFYA YATINGA ROBO FAINALI - SHIMIWI
      • SAGCOT CEO meets with the US journalists
      • Redd’s Miss Tanzania 2013/14 atembelea TBL leo
      • KONGAMANO LA WAZEE WASTAAFU LAFANYIKA ZANZIBAR
      • ufunguzi Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Taasis...
      • AJALI ZAPUNGUA MKOANI IRINGA
      • MWAKALEBELA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU 13 M...
      • MAALIM SEIF AWATAKA WAISLAM NCHINI KUUNGA NA KUSHI...
      • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMIRI J...
      • Japanese Grant for the Food Security Project for U...
      • ACCT members attending Master Builders South Afric...
      • Awamu ya pili ya chakula cha hisani cha Taasisi ya...
      • MHE. MWIGULU NCHEMBA AWAKUNA WENGI DMV.
      • MWENGE WAZINDUA UJENZI WA OFISI YA KATA TANDALA WI...
      • WAZIRI CHIKAWE ATEMBELEA GEREZA KUU LA ISANGA,MKOA...
      • MKUTANO WA CCM CHWAKA UNGUJA
      • TAARIFA YA MSIBA
      • SingTel Group and Samsung partner to enhance mobil...
      • TIC yawahakikishia wawekezaji ushirikiano zaidi
      • DIAMOND ALIVYOWAKUNA MASHABIKI WAKE NDANI YA GOLD ...
      • KAPOTIVE STAR SINGER-S BUKOBA KUWASHA MOTO JIJINI ...
      • TFDA YAENDESHA KAMPENI YA UTUMIAJI WA VYAKULA VILI...
      • Wakazi wa eneo la hifadhi ya Ngorongoro wapokea ch...
      • AZANIA BANK YACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI SHULE Y...
      • United States 2015 Diversity Visa Program Now Open
      • OPERESHENI KIMBUNGA AWAMU YA PILI YASHIKA KASI KAT...
      • mdau mugassa mwenda ahojiwa na BBC kwa kufurahishw...
      • Airtel yawanoa maafisa waTRA jinsi ya kulipia ada ...
      • NAIBU WAZIRI FEDHA AKAGUA UJENZI WA BARABARA VISIW...
      • 2013 Young Achievers Awards Nomination Open!
      • No title
      • IN LOVING MEMORY of DORA HOSEA TALAWA 1ST ANNIVESSARY
      • ngoma azipendazo ankal
      • TAARIFA YA MSIBA WA MAMA ROSE HEINRICH SANGIWA MATAJI
      • FRANSIC MIYEYUSHO AMTWANGA SADIK MOMBA KWA POINTI
      • Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Wafanyakazi...
      • Mahojiano ya JK na radio ya umoja wa mataifa, New ...
      • J&M Virgo washusha mali mpya
      • Daktari wa Rais Kikwete kupima afya na kuwapa lese...
      • MWENGE WA UHURU WATUA MAKETE
      • Swali la kizushi: Je ni mkono upi unaofaa kuvalia ...
      • No title
      • No title
      • introducing Mchaga na pesa by KiwaStrond ft. Banx
      • bwawa la maini oye! Suarez arudi na kupiga bee kat...
      • HARAMBEE KUCHANGIA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KUS...
      • introducing 'Ni Noma' by Go Getta of the night cra...
      • MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ...
      • Ubalozi wetu zambia na wajisiriamali wa Tanzania w...
      • Grace aikaeli Mbowe na mumewe wafariki kwa ajali ...
      • Simba yaibanjua Ruvu JKT 2-0 leo neshno
      • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMA...
      • ZUMBA KUKWE AMSHINDA HAMADUU MWALIMU KWA KO RAUNDI...
      • TANZIA: Msiba wa Bi ROSE HENRISCH SANGIWA MATAJI
      • Sherehe za kufunga mafunzo katika kikosi cha 842 ...
      • Benki ya posta Tanzania tawi la Songea yaipiga jek...
      • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHING...
      • TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO NI KWELI KWAMBA LIMEPOTE...
      • No title
      • Tanzanian Minister of Defence Meets Governor of So...
      • UPANUZI WA BARABARA YA BENDERA TATU HADI KAMATA KU...
      • MISS UTALII TANZANIA KUTANGAZA NYATI WA AJABU NA ...
      • Cheka unenepe
      • WAFANYAKAZI WA IDARA MBALI MBALI ZA SERIKALI WACHU...
      • Kiwanda cha kuzalisha malighafi za kutengeneza Gil...
      • MAMA SALMA KIKWETE APEWA URAIA WA HIARI WA JIMBO L...
      • MKUTANO WA SIKU TATU WA MAOFISA WA JUU WA JESHI LA...
      • NBC YATENGA SIKU MAALUMU KUWASHUKURU WATEJA WAO
      • Serikali yabariki tamasha la Utamaduni Handeni
      • Matukio zaidi ya Mhe. Rais Kikwete alipolihutubia ...
      • ngoma azipendazo ankal
      • chemsha bongo...
      • cassim mganga akitumbuiza kwenye tamasha la fiesta...
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile