50 Bing Coupons

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Thursday, 19 September 2013

WAZIRI MKUU AZINDUA MFUMO WA UFATILIKI WA ASALI YA TANZANIA

Posted on 11:53 by Unknown
Taasisi ya GS1 Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la Uwezeshaji (NEEC) wamezindua mfumo wa ufatiliki wa asali ya Tanzania (Honey Traceability Project).

Sherehe za uzinduzi wa mfumo huo muhimu kwa bidhaa zinazozalishwa nchini umefanywa mjini Dodoma na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyewakilishwa na Waziri wa Uwezeshaji Dr.Mary Nagu. Katika salamu zake kwa wadau Mheshimiwa Waziri Mkuu amewataka wasimamizi wa mfumo huo kuhakikisha unaanza mara moja ili kuiwezesha asali ya Tanzania iweze kuuzwa nje ya nchi na kuwanufaisha wakulima.

Kwa kuwa na mifumo hii, kutaziwezesha bidhaa za Tanzania zinaweza kuuzwa kama finished products nje ya nchi, kwani mifumo hii ua ufatiliki (Traceability System) inaweza kuonyesha historia ya bidhaa kuanzia ikiwa shambani, ilipopitia mpaka inamfikia mlaji, taarifa ambazo zikifuatiliwa zinapatikana kwa urahisi.

Awali Mkurugenzi mkuu wa GS1 Tanzania Bi. Fatma Kange alisema kuwa GS1 imejikita katika kutengeneza mifumo ya Ufatiliki (Traceability System) dunia nzima, tangu imeanzishwa miaka 40 iliyopita na kwa Tanzania mfumo huu ni wa kwanza wa kidigitali, kwani mpaka sasa ni mazao mawili tuu ya Tanzania ndio yamo kwenye mfumo wa ufatiliki ambayo ni Minofu ya Samaki na Mfumo wa Ufatiliki wa Kahawa.

Aidha akizungumza kwenye uzinduzi huo, mtaalamu wa mifumo ya Ufatiliki ya GS1 Tanzania Bw. Pius Mikongoti alisema kuwa Tanzania haina hiyari ya kuingia kwenye mifumo hii ya ufatiliki kwani kwa mujibu wa Sheria ya Chakula na MAdawa ya Jumuiya ua Ulaya, sheria no 78 ya mwaka 2002 inasema kuwa bidhaa zote zinazoliwa na binadamu ama mifuko katika jumuiya hiyo ni lazima ziwemo kwenye mifumo ya Ufatiliki ili ziweze kujulikana zilipotoka kuanzia mtengenezaji wa kwanza hadi zinapomfikia mlaji, hii ni katika kuzilinda haki za mlaji.

“Nia ni kuzalisha asali yenye viwango vya kimataifa hata kama ni ya kuliwa hapa hapa nchini lakini lazima iwe kwenye viwango ambavyo unaweza kuuza popote” alisema Bi. Kange

Naye Mheshimiwa Abdallah Kigoda, Waziri wa Viwanda na Biashara alisema kuwa kwa sasa sekta ya asali inakumbwa na changamoto nyingi ikiwamo ukosefu a vifungashio, masoko hafifu na vifaa vya urinaji na uchakataji wa kisasa, Kupitia wizara ya Viwanda na Bishara, serikali imefanikiwa kuongea na Kampuni kadhaa zikiwamo Kioo Limited na Omar Packaging ambazo zimekubali kuzalisha vifungashio maalumu kwa ajili ya zao hilo la asali.

Naye Mheshimiwa Nagu amesema kuwa Serikali kupitia baraza la Uwezeshaji na Wizara yake ya Uwezeshaji watahakikisha mifumo hii ya Ufatiliki inatengenezwa kwenye mazao yote ya Tanzania jambo ambalo litamaliza uuzwaji wa bidhaa ghafi sokoni.

Katika salamu zao kwa wadau kwenye uzinduzi huo Taasisi ya TPSF ambayo ni moja ya taasisi mama za GS1 imesema kuwa inajivunia kuona ndani ya miaka miwili tokea uanzishwaji wake Taasisi hii ya GS1 imeanza kuleta matunda stahiki kwa Watanzania, na hivyo kuahidi kuendelea kuisaidia taasisi hii na sekta binafsi kwa ujumla ili kuleta maendeleo ya TAifa kwa ujumla.

Nalo shirika la Viwango ambalo ni mmoja wa wadau na ndio waliofadhili uzinduzi hu mjini Dodoma wamesema kuwa kwa upande wao wameshatengeneza kiwango cha asali ambacho kinakubalika duniani kote na hivyo kuifanya kazi ya utengenezaji wa mfumo huo kuwa rahisi.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Wakuu wa Mikoa ya Katavi, Manyara, Dodoma, Singida na Tabora na Wakuu kadhaa wa Wilaya za mikoa husika, Wabunge, Wakurugenzi wa Maendeleo wa Mikoa na Wilaya, maafisa nyuki, na wadau mbali mbali wa nyuki hudu mashirika kadhaa yakiwakilishwa kama Word Vision, PASS, Shirika la Viwango la Taifa, Taasisi ya Sekta Binafsi, Benki ya Rasilimali, Taasisi ya NMB Foundations for Agriculture.

Mfumo huu kwa kuanzia umelenga mikoa Kumi ikiwamo Morogoro, Pwani, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Katavi, Kigoma na Rukwa, na Tabora. Baada ya uzinduzi washiriki walipata nafasi ya kutembelea shamba la Mheshimiwa Waziri Mkuu lililoko endeo la Zuzu nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Ukwekezaji, Dr. Mary Nagu akikata utepe kuzindua Mfumo wa Ufatiliki (Traceability System) wa Asali ya Tanzania, Wa kwanza kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Abdallah Kigoda, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anayeangalia kushoto kwa Waziri Nagu ni Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania Elibariki Mmari na kushoto kwake ni Fatma Kange, Afisa Mtendaji Mkuu wa GS1 Tanzania.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • tamasha la 32 la sanaa la bagamoyo lawasha moto, Mhe Makala asema utamaduni ni ajira kwa vijana
    NAIBU Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makala amesema Sanaa na Utamaduni nchini itaendelea kuenziwa ili kuwaleta a...
  • wadau farida na paul wameremeta
     Wakila pozi baada ya kumeremeta katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam kabla ya kwenda kwenye mnuso wao wa nguvu katika hote...
  • WAZIRI DK. NCHIMBI AMTEMBELEA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI HOSPITALI YA MUHIMBILI LEO
    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Pa...
  • Naibu Spika aongoza Mkutano wa ACP nchini Ubelgiji
    Mhe.Job Ndugai,Mbunge wa Kongwa na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania akiongoza Mkutano wa Kamati ya Mazingira na Jamii cha Umoja wa Mabunge y...
  • Sherehe za kufunga mafunzo katika kikosi cha 842 Kj Mlale Jkt, Songea
      Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Mhe Senyi Ngaga kushoto akiangalia shehena ya mahindi ya chakula katika kikosi cha 842 Kj mlale Jkt...
  • barabara ya Mtoni-mbagala ilivyo
  • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMANI TANZANIA
     Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akishiriki kuwasha mshumaa kama tendo la kuiangaza nchi ya Tanzania.  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape ...
  • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHINGTON, DC YAFANA
    Katibu wa Jumuiya ya Tanzania akielezea nini maana ya GLN na kwanini Jumuiya ya Tanzania DMV ni moja ya washiririki  Banda la Tanzania lilki...
  • BACK TO THE SUA SEASON 2 EPISODE 2, KIJENGE, ARUSHA
    YECHU! YECHU! YECHU! HII HAILIPIWI HATA KUMI ARIFU  YAANI KIINGILIO NDO KITU HAMNAGA Pale Pale fasi ya K-JUU mwisho wa daladala mkabala na k...
  • IN LOVING MEMORY of DORA HOSEA TALAWA 1ST ANNIVESSARY
    28 th September 2013 marks the first year of the passing away of our beloved mum.  Memories continue to linger around us because there are ...

Blog Archive

  • ▼  2013 (500)
    • ►  October (22)
    • ▼  September (478)
      • HIKI HAPA KILIO CHA WANAFUNZI WA UDAKTARI BUGANDO...
      • No title
      • BREKING NYUUZZZZZZ: SERIKALI YA MAREKANI YAFUNGA S...
      • No title
      • NATURAL PRODUCTS FOR your skin
      • SIKU YA UTALII DUNIANI YENYE KAULI MBIU UTALII NA ...
      • President Kikwete sends Congratulatory Message to ...
      • WAKAZI WA KIKUYU KUSINI WAANDAMANA KUPINGA BOMOABO...
      • ngoma azipendazo ankal
      • wadau farida na paul wameremeta
      • ACCT members attend Master Builders South Africa C...
      • magari yanauzwa
      • Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali Bw L...
      • Spika Makinda apongeza Mabunge ya Afrika kwa kuong...
      • KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA JOHN CASMIR MINJA AH...
      • dk shein aagana na balozi wa marekani aliyemaliza ...
      • KATIBU MKUU UTUMISHI, Bw. GEORGE YAMBESI AFUNGUA M...
      • Maalim Seif aifunga rasmi Ijtimai ya Kimataifa ili...
      • HOJA YA HAJA: TUIENZI AMANI YETU KWA GHARAMA YOYOT...
      • MWIGULU NCHEMBA KUNDURUMA NDANI YA LONDON UINGEREZA
      • mwenge wa uhuru watua jijini mbeya
      • MBUNGE WA VITI MAALUMU TABORA,MH MUNDE TAMBWE ADHA...
      • JK arejea nyumbani kutoka Canada na Marekani
      • JK alipohudhuria Mkutano wa Kukabiliana na Ujangil...
      • Globu ya Jamii yakuletea Exclusive Intavyuuu na Re...
      • KANYABOYA LINGINE LAIBUKA DAR,WADAU KAENI CHONJO
      • WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU AIPONGEZA VODA...
      • TIMU YA WIZARA YA AFYA YATINGA ROBO FAINALI - SHIMIWI
      • SAGCOT CEO meets with the US journalists
      • Redd’s Miss Tanzania 2013/14 atembelea TBL leo
      • KONGAMANO LA WAZEE WASTAAFU LAFANYIKA ZANZIBAR
      • ufunguzi Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Taasis...
      • AJALI ZAPUNGUA MKOANI IRINGA
      • MWAKALEBELA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU 13 M...
      • MAALIM SEIF AWATAKA WAISLAM NCHINI KUUNGA NA KUSHI...
      • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMIRI J...
      • Japanese Grant for the Food Security Project for U...
      • ACCT members attending Master Builders South Afric...
      • Awamu ya pili ya chakula cha hisani cha Taasisi ya...
      • MHE. MWIGULU NCHEMBA AWAKUNA WENGI DMV.
      • MWENGE WAZINDUA UJENZI WA OFISI YA KATA TANDALA WI...
      • WAZIRI CHIKAWE ATEMBELEA GEREZA KUU LA ISANGA,MKOA...
      • MKUTANO WA CCM CHWAKA UNGUJA
      • TAARIFA YA MSIBA
      • SingTel Group and Samsung partner to enhance mobil...
      • TIC yawahakikishia wawekezaji ushirikiano zaidi
      • DIAMOND ALIVYOWAKUNA MASHABIKI WAKE NDANI YA GOLD ...
      • KAPOTIVE STAR SINGER-S BUKOBA KUWASHA MOTO JIJINI ...
      • TFDA YAENDESHA KAMPENI YA UTUMIAJI WA VYAKULA VILI...
      • Wakazi wa eneo la hifadhi ya Ngorongoro wapokea ch...
      • AZANIA BANK YACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI SHULE Y...
      • United States 2015 Diversity Visa Program Now Open
      • OPERESHENI KIMBUNGA AWAMU YA PILI YASHIKA KASI KAT...
      • mdau mugassa mwenda ahojiwa na BBC kwa kufurahishw...
      • Airtel yawanoa maafisa waTRA jinsi ya kulipia ada ...
      • NAIBU WAZIRI FEDHA AKAGUA UJENZI WA BARABARA VISIW...
      • 2013 Young Achievers Awards Nomination Open!
      • No title
      • IN LOVING MEMORY of DORA HOSEA TALAWA 1ST ANNIVESSARY
      • ngoma azipendazo ankal
      • TAARIFA YA MSIBA WA MAMA ROSE HEINRICH SANGIWA MATAJI
      • FRANSIC MIYEYUSHO AMTWANGA SADIK MOMBA KWA POINTI
      • Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Wafanyakazi...
      • Mahojiano ya JK na radio ya umoja wa mataifa, New ...
      • J&M Virgo washusha mali mpya
      • Daktari wa Rais Kikwete kupima afya na kuwapa lese...
      • MWENGE WA UHURU WATUA MAKETE
      • Swali la kizushi: Je ni mkono upi unaofaa kuvalia ...
      • No title
      • No title
      • introducing Mchaga na pesa by KiwaStrond ft. Banx
      • bwawa la maini oye! Suarez arudi na kupiga bee kat...
      • HARAMBEE KUCHANGIA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KUS...
      • introducing 'Ni Noma' by Go Getta of the night cra...
      • MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ...
      • Ubalozi wetu zambia na wajisiriamali wa Tanzania w...
      • Grace aikaeli Mbowe na mumewe wafariki kwa ajali ...
      • Simba yaibanjua Ruvu JKT 2-0 leo neshno
      • KANISA LA TGMIT LAFANYA IBADA MAALUMU KUIOMBEA AMA...
      • ZUMBA KUKWE AMSHINDA HAMADUU MWALIMU KWA KO RAUNDI...
      • TANZIA: Msiba wa Bi ROSE HENRISCH SANGIWA MATAJI
      • Sherehe za kufunga mafunzo katika kikosi cha 842 ...
      • Benki ya posta Tanzania tawi la Songea yaipiga jek...
      • GLOBAL LANGUAGE NETWORK (GLN) ILIYOFANYIKA WASHING...
      • TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO NI KWELI KWAMBA LIMEPOTE...
      • No title
      • Tanzanian Minister of Defence Meets Governor of So...
      • UPANUZI WA BARABARA YA BENDERA TATU HADI KAMATA KU...
      • MISS UTALII TANZANIA KUTANGAZA NYATI WA AJABU NA ...
      • Cheka unenepe
      • WAFANYAKAZI WA IDARA MBALI MBALI ZA SERIKALI WACHU...
      • Kiwanda cha kuzalisha malighafi za kutengeneza Gil...
      • MAMA SALMA KIKWETE APEWA URAIA WA HIARI WA JIMBO L...
      • MKUTANO WA SIKU TATU WA MAOFISA WA JUU WA JESHI LA...
      • NBC YATENGA SIKU MAALUMU KUWASHUKURU WATEJA WAO
      • Serikali yabariki tamasha la Utamaduni Handeni
      • Matukio zaidi ya Mhe. Rais Kikwete alipolihutubia ...
      • ngoma azipendazo ankal
      • chemsha bongo...
      • cassim mganga akitumbuiza kwenye tamasha la fiesta...
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile